WIMBO WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI
Ee Mungu twaomba uilinde
Jumiya Afrika Mashariki
Tuwezeshe Kuishi kwa amani
Tutimize na malengo yetu.
Jumuiya Yetu sote tuilinde
Tuwajibike tuimarike
Umoja wetu ni nguzo yetu
Idumu Jumuiya yetu.
Uzalendo pia mshikamano
Viwe msingi wa Umoja wetu
Na tuilinde uhuru na Amani
Mila zetu na desturi zetu.
Viwandani na hat mashambani
Tufanye kazi sote kwa makini
Tujitoe kwa hali na mali
Tuijenge Jumuiya bora.
For more information visit the official East African Community:
http://www.eac.int/about/emblem