WIMBO WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI

Ee Mungu twaomba uilinde

Jumiya Afrika Mashariki

Tuwezeshe Kuishi kwa amani

Tutimize na malengo yetu.

 

Jumuiya Yetu sote tuilinde

Tuwajibike tuimarike

Umoja wetu ni nguzo yetu

Idumu Jumuiya yetu.

 

Uzalendo pia mshikamano

Viwe msingi wa Umoja wetu

Na tuilinde uhuru na Amani

Mila zetu na desturi zetu.

 

Viwandani na hat mashambani

Tufanye kazi sote kwa makini

Tujitoe kwa hali na mali

Tuijenge Jumuiya bora.

 

For more information visit the official East African Community:

http://www.eac.int/about/emblem